Subscribe Us

Header Ads

Urusi ina silaha ngapi za nyuklia?



Rais Putin ameviweka vikosi vya nyuklia vya Urusi katika tahadhari "maalum", na kuzua wasiwasi kote ulimwenguni.


Lakini wadadisi wa mambo wanadokeza kwamba hatua zake huenda zikatafsiriwa kuwa onyo kwa nchi nyingine kutozidisha ushiriki wao nchini Ukraine, badala ya kuashiria kutaka kutumia silaha za nyuklia.


Silaha za nyuklia zimekuwepo kwa takriban miaka 80 na nchi nyingi zinaziona kama kizuizi kinachoendelea kudhamini usalama wa taifa lao.


Urusi ina silaha ngapi za nyuklia?

Takwimu zote za silaha za nyuklia ni makadirio lakini, kwa mujibu wa Shirikisho la Wanasayansi wa Marekani, Urusi ina vichwa vya nyuklia 5,977 - vifaa vinavyosababisha mlipuko wa nyuklia - ingawa hii inajumuisha takriban 1,500 ambazo zimechoka na zinatazamiwa kuvunjwa.


Kati ya 4,500 zilizosalia au zaidi, nyingi zinachukuliwa kuwa silaha za kimkakati za nyuklia - makombora ya balestiki, au makombora, ambayo yanaweza kulengwa kwa umbali mrefu. Hizi ndizo silaha ambazo kawaida huhusishwa na vita vya nyuklia.



Zilizosalia ni silaha ndogo za nyuklia zisizoweza kuharibu sana kwa matumizi ya masafa mafupi kwenye uwanja wa vita au baharini.


Lakini hii haimaanishi kuwa Urusi ina maelfu ya silaha za nyuklia za masafa marefu tayari kwenda.


Wataalamu wanakadiria takribani vichwa 1,500 vya kivita vya Urusi kwa sasa "vimetumwa", kumaanisha kuwa viko kwenye kambi za makombora na mabomu au kwenye manowari baharini.


Je, hii inalinganishwaje na nchi nyingine?

Nchi tisa zina silaha za nyuklia: China, Ufaransa, India, Israel, Korea Kaskazini, Pakistan, Russia, Marekani na Uingereza.



China, Ufaransa, Urusi, Marekani na Uingereza pia ni miongoni mwa mataifa 191 yaliyosaini Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Silaha za Nyuklia (NPT).


Chini ya makubaliano hayo, wanapaswa kupunguza akiba yao ya silaha za nyuklia na, kwa nadharia, wamejitolea kutokomeza kabisa.


Na imepunguza idadi ya vichwa vya kivita vilivyohifadhiwa katika nchi hizo tangu miaka ya 1970 na 80.


India, Israel na Pakistan hazikuwahi kujiunga na NPT - na Korea Kaskazini iliondoka mwaka 2003.


Israel ni nchi pekee kati ya tisa ambayo haijawahi kukiri rasmi mpango wake wa nyuklia - lakini inakubaliwa na wengi kuwa na vichwa vya nyuklia.


Ukraine haina silaha za nyuklia na, licha ya shutuma za Rais Putin, hakuna ushahidi kuwa imejaribu kuzipata.


Silaha za nyuklia zina uharibifu gani?

Silaha za nyuklia zimeundwa kusababisha uharibifu mkubwa zaidi.


Kiwango cha uharibifu hutegemea mambo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na:


• Ukubwa wa kichwa cha silaha


• Jinsi inavyolipua juu ya ardhi


• Mazingira ya ndani



Lakini hata kichwa kidogo cha silaha ya kivita kinaweza kusababisha upotezaji mkubwa wa maisha na matokeo ya kudumu.

Bomu lililoua hadi watu 146,000 huko Hiroshima, Japan, wakati wa Vita vya pili vya dunia, lilikuwa kilotoni 15.

Na vichwa vya nyuklia leo vinaweza kuwa zaidi ya kilotoni 1,000.

Kidogo kinatarajiwa kuishi katika eneo la athari la mlipuko wa nyuklia.

Baada ya mwanga wa kupofusha, kuna moto mkubwa na wimbi la mlipuko ambalo linaweza kuharibu majengo na miundombinu kwa kilomita kadhaa.

Je, 'kizuizi cha nyuklia' kinamaanisha nini na kimefanya kazi?
Hoja ya kudumisha idadi kubwa ya silaha za nyuklia imetokana na uwezo wa kuwaangamiza kabisa adui yako ingewazuia kukushambulia.

Neno marufu zaidi kuelezea hili likawa uharibifu wa uhakika (Mad).

Ijapokuwa kumekuwa na majaribio mengi ya nyuklia na ongezeko la mara kwa mara la utata wa kiufundi na nguvu za uharibifu, silaha nza nyuklia hazitumiwi katika mapambano ya silaha tangu 1945.

Sera ya Urusi pia unazuia matumizi ya silaha za nyuklia na kuorodhesha hatu anne zinazoweza kuruhusu utumizi wa sillaha hizo: