Subscribe Us

Header Ads

Wanajeshi wa Urusi kati ya 2,000 na 4,000 wameuawa Ukraine, Marekani yasema

 



Urusi imekumbwa na vifo vingi vya wanajeshi wake kati ya 2,000 na 4,000 nchini Ukraine, mkuu wa idara ya ujasusi ya Marekani ameliambia bunge la Marekani.


"Walikuwa na mpango mbaya," Scott Berrier alisema, wakati akikadiria, kwa ujasiri mdogo, vifo kulingana na taarifa za usalama na vyanzo vingine.


Maelezo hayo yanafuatia ripoti za awali, kutoka wizara ya ulinzi ya Ukrania, kwamba kamanda wa ngazi ya juu wa jeshi la Urusi aliuawa katika mapigano makali katika mji wa mashariki wa Ukraine wa Kharkiv.