Subscribe Us

Header Ads

Marekani kuweka katika tahadhari timu ya nyuklia



Marekani itaweka katika tahadhari kikosi cha usaidizi cha nyuklia (NEST). Uamuzi huu ulifanywa na Waziri wa nishatiJ ennifer Granholm baada ya mazungumzo ya dharura na Ukraine.


NEST kikundi cha wanasayansi, mafundi na wahandisi ambao kazi yao ni kujibu haraka iwezekanavyo aina yoyote ya tisho la nyuklia kokote duniani.


"Operesheni ya jeshi la Urusi katika eneo la nyuklia ni uzembe kabisa na lazima usitishwe ," alisema, na kuongeza kuwa mitambo ya nyuklia imelindwa na mifumo imara na inafungwa kwa usalama.


" Hatuoni viwango vya hali ya juu vya mionzi ya nyuklia karibu na eneo ," Granholm alisema.