Awali tuliripoti juu ya kuzuiwa kwa matangazo ya shirika la utangazaji la Uingereza BBC News nchini Urusi.
Lakini sasa shirika la utangazaji la Ujerumani Deutsche Welle (DW) nalo limepigwa marufuku nchini Urusi.
Mamlaka ya Urusi imeizuia mtandao wa DW.
Urusi ilikuwa tayari imepiga marufuku huduma ya DW ya Urusi kutangaza na kuondoa kibali kutoka kwa wanahabari wake mwezi uliopita, kabla ya uvamizi wa Ukraine.