Mshindi wa pili Rafal Trzaskowski kutoka chama cha Jukwaa la Kiraia PO, alikuwa na asilimia 28.92, na hivyo kufaulu kuingia katika duru ya pili ya uchaguzi utakaofanyika Julai 12.
Mgombea binafsi Rafal Holownia alishika nafasi ya tatu kwa kupata asilimia 13.69, huku wagombea wengine wanane wakishindwa kufikisha asilimia 10.
Kampeni za uchaguzi huo ziligubikwa na wasiwasi kuhusu mmomonyoko wa haki za kidemokrasia pamoja na masuala ya kiuchumi.
